Karibu!
Karibu katika kanisa la Waadventista Wasabato - Mlimani. Ibada zetu ni kila Sabato Jumamosi, Karibu ujiunge tushiriki wote kwa pamoja katika kujifunza neno la Bwana wetu Yesu Kristo. Wakaribishe ndugu, jamaa, rafiki na familia kwa ujumla.
Mathayo 11: 28-30 - "Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu, kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi."
Kutuhusu
Karibu jimbo kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania. Sisi ni sehemu ya Kanisa la Waadventista wa sabato ambayo ni jamii ya watu waliokusudia kukuza uhusiano wa karibu kabisa na Mungu pamoja na kuwa na mwenendo kama aliokuwa nao Yesu. Kiini cha utume wetu ni kuushuhudia ulimwengu juu ya tumaini pekee lenye baraka linalotokana na uzoefu binafsi wa mahusiano bora na Mungu Mwokozi wetu mwenye Upendo, na kujiandaa kwa tukio kubwa kabisa la marejeo yake ambayo yamekaribia sana.
Kanisa la Waadventista wa sabato linajitambua kuwa kanisa la masalio la unabii wa Biblia wa siku za mwisho. Washiriki wa kanisa hili kwa pamoja huelewa jukumu lao maalumu kama mabalozi wa ufalme wa Mungu, na wajumbe wa marejeo ya Yesu Kristo yaliyo karibu. Waadventista wasabato wamejiandikisha kama jeshi la wafanyakazi pamoja na Mungu katika utume wa kuurejesha ulimwengu kutoka katika nguvu na uwepo wa uovu, kama sehemu ya pambano kuu baina ya Kristo na Shetani. Kwa hiyo, kila hali ya maisha ya mshiriki wa Kanisa huathiriwa na kusadiki na kuamini kuwa tunaishi katika siku za mwisho za unabii wa Biblia na kwamba kurudi kwa Yesu Kristo kuko karibu sana. Waadventista wasabato wameitwa na Mungu kuishi katika ulimwengu huu. Kila tendo la maisha ya Mkristo hufanyika “katika jina la Yesu” na kutangaza ufalme wake.
UTUME WA KANISA
Utume wa Kanisa la Waadventista wa Sabato ni kuwafanya watu wote wawe wanafunzi wa Yesu, kutangaza injili ya milele katika Ujumbe wa maliaka wa tatu, Ufunuo 14:6-12, na kuuanda ulimwengu kwa marejeo ya Kristo yaliyo karibu.
UTEKELEZAJI WA UTUME WETU
Kwa kuongozwa na biblia na roho mtakatifu, waadventista wasabato hutekeleza utume huu kupitia maisha yanayoakisi alivyoishi Kristo, katika kuwasiliana, kufanya wanafunzi, kufundisha, kuponya na kuhudumia.
NJOZI YA UTUME WETU
Kwa kupatana na mafunuo ya Biblia, Waadventista wa Sabato tunauona utume wetu ukifikia kilele katika mpango wa Mungu wa urejeshwaji wa viumbe vyake katika ukamilifu wa mapenzi yake na haki yake.
Ratiba ya Ibada
Karibu tushirikiane katika vipindi vyetu mbalimbali vya ibada kila wiki.
Jumatano
Ibada ya Maombi
17:00 Hrs - 18:00 Hrs
Ijumaa
Kufungua Sabato
18:00 Hrs - 19:00 Hrs
Jumamosi
Ibada Kuu
09:00 Hrs - 18:00 Hrs
Viongozi
.
Jina: Abednego Masanja
Wadhifa: Mzee wa kanisa
Jina: Angallo Angallo
Wadhifa: Mzee wa kanisa
Jina: Omary Mbwambo
Wadhifa: Mzee wa kanisa
Jina: Steven Senjiro
Wadhifa: Mzee wa kanisa